- Gavana wa Machakos Alfred Mutua ameahidi kumsaidia mzee mmoja kutoka kaunti ya Nyeri na familia yake ambao wanaishi maisha ya ufukara
- Mutua alimtembelea mzee Muchoki alipokuwa katika ziara zake kaunti hiyo
- Mzee Muchoki yuko na tatizo la kutoona na anaishi kwenye nyumba iliyojengwa kwa mbao pamoja na mke wake
-Aidha, Mutua aliahidi kugharamia matibabu kwa macho ya Muchoki ambapo atasafirishwa jiji Nairobi
Gavana wa Machakos Alfred Mutua alimtembelea mzee ChristoPher Maina Muchoki na mkewe Ann Gathigia Jumamosi Aprili 8 katika kijiji cha Irui eneo bunge la Mathira.
Habari Nyingine: Unawajua magaidi hawa? Polisi wana zawadi yako ya KSh 16 milioni!

Mutua ambaye alikuwa katika ziara rasmi kaunti ya Nyeri, alisema kuwa aliguswa sana alipoona maisha ya ufukara anayoyaisha mzee Muchoki pamoja na mkewe.
Habari Nyingine: https://kiswahili.tuko.co.ke/270483-unawajua-magaidi-hawa-polisi-wana-zawadi-yako-ya-ksh-16-milioni.html#270483
" Wanaishi katika nyumba chakavu ambayo imejengwa kwa mbao na udongo kwenye sakafu, hii ilinikumbusha maisha ambayo niliwahi ishi nikiwa mchanga," Mutua alisema.

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Kilichomfurahisha Mutua zaidi ni pale ambapo Muchoki alisema kuwa yeye hukuwa shabiki wake tangu enzi za rais mstaafu Mwai Kibaki ambapo alikuwa msemaji wa serikali.
Habari Nyingine: Mambo 13 ya kushangaza ambayo wanawake Wakenya hufanya katika mahusiano yao ya kwanza ya kimapenzi
Kando na kuwa maskini,Muchoki pia yuko na tatizo la kuona na gavana Mutua ameahidi kugharamia matibabu yake.

" Jumanne ijayo nitamtuma dereva na gari langu aende kumchukua Muchoki na mama mwingine kipofu ili wapelekwe hositalini watibiwa na daktari wa macho," Mutua aliandika Facebook.

Mutua pia aliahidi kwamba atashirikiana na mke wake Lilian kumjengea Muchoki nyumba kutumia mbinu mwafaka ya Chap Chap Technology.

Habari Nyingine: Unamjua vyema mwakilishi wa kike wa Murang’a Sabina Chege? Pata uhondo

Read: ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibH14gJFmnpqukaOubq3Ln6menF2iwrXBwGaYoqyVoq%2BmuMSaZJ%2BZnZ65qq2Mppiso5mjtm63wK6lraFdrq5uutieqaJmmKm6rQ%3D%3D